Na Esther Macha, TimesmajiraOnline, Rungwe
KATIKA kuhakikisha wanawake wanajikomboa kiuchumi katika nyanja mbalimbali za kuachana na dhana ya kuwa tegemezi,Naibu Waziri wa maji ambaye pia Mbunge wa vitimaalum mkoa wa Mbeya, Mhandisi Maryprisca Mahundi amezidi kuyafikia makundi mbalimbali kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi .
Kikundi kimojawapo kilichofikiwa na mkono wa kheri ni kikundi cha Mwanamke Shujaa cha Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambacho kimechangiwa Mil.5 kwa ajili ya ujenzi wa mabanda ya kufugia mifugo .
Mhandisi Mahundi katika hafla hiyo ya maadhimisho ya sikukuu ya wanawake alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika Kiwilaya Tukuyu mjini ambapo lengo lilikuwa kupata mil.20 ili waweze kufikia malengo .
Mahundi amechangia zaidi ya mi.3 akiwa ameungwa mkono na rafiki zake.
Lengo la Mahundi ni kuhakikisha wanawake wanamiliki uchumi wao akitekeleza kauli mbiu yake ya “Twende Tukue Pamoja”

More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo