Na Joyce Kasiki, TimesMajira,Online, Dodoma
RAIS John Magufuli anatarajiwa kulihutubia Bunge Ijumaa, hotuba ambayo inatarajia kuonesha dira ya Serikali yake katika kipindi uongozi wake wa pili cha miaka mitano katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Kupitia hotiba hiyo Rais Magufuli anatarajia kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ratiba ya Rais Magufuli kuhutubia Bunge imetolewa leo na Spika wa Bunge, Job Ndugai wakati akizungumza bungeni kuhusu utaratibu utakavyokuwa kesho kutwa.
“Hotuba hii ni muhimu, lakini kupitia sisi wabunge anakuwa analihutubia Taifa, kwa hiyo naomba niwataarifuni kuwa kesho kutwa saa tatu kamili asubuhi tutawaomba waheshimiwa wote tuwe ndani ya ukumbi huu,” amesema Spika Ndugai.
More Stories
Serikali ,Washirika wa Maendeleo waweka mkakati utekelezaji Dira ya 2050
Benki ya Exim yazindua suluhisho la malipo ya kisasa kwenye Z- Summit 2025
DCEA yateketeza zaidi ya ekari 300 za bangi