Na Joyce Kasiki,TimesMajira Online,Dodoma
MBUNGE wa Kilombero, Peter Lijualikali amesema,Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ina taarifa zote za matumizi ya fedha za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hivyo inachofanya kuwahoji wabunge na viongozi wengine ni kutaka kupata uhakika.
Lijualikali ambaye ameshaomba kuhamia CCM mara baada ya Bunge la 11 kuvunjwa ,ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi mara baada ya kutoka kuhojiwa na TAKUKURU.
Kufuatia hali hiyo amewaasa wahojiwa wote kueleza ukweli wa kile wanachokijua kwani hata wakidanganya haitasaidia kitu.
Lijualikali ambaye ameingia katika mahojiano saa 2:20 asubuhi na kutoka saa 5:5 asubuhi amesema,wahojiwa wasiwe na hofu kwani mahojiano ni ya kirafiki na hakuna kitu kipya zaidi ya wanachokijua.
More Stories
Rais Samia alivyotunukiwa tuzo ya uchumi Uturuki, azidi kutwaa tuzo za kimataifa
Habari picha: Mbunge wa Malinyi uso kwa uso na Waziri Mkuu Bungeni
Mbunge aiangukia Serikali isaidie wananchi waliokumbwa na mafuriko Kigoma