October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Kidemokrasia ya KoreaKim Jong-un (kulia) amemkaribisha Donald Trump, Rais wa Maerkani nchini North Korea. Picha ya The Guardian

Kim Jong Un azidi kuzua hofu Marekani, Korea, Japan

PYONYANG, Majasusi wa Korea ya Kusini na Marekani wamethibitisha kuwa,silaha mpya ya kimkakati iliyotajwa na kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Kidemokrasia ya Korea, Kim Jong Un mwishoni mwa mwaka jana tayari imeundwa na inaonyesha kuwa ni tishio la usalama.

Wamesema,manowari mpya ya tani 3,000 yenye vifaa vingi vya makombora imezinduliwa na kikosi maalum cha SLBM.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Dong-a Ilbo linalochapishwa nchini Korea Kusini limedai katika ripoti yake kuwa, Korea Kaskazini imeshafanikiwa kuunda makombora hayo ya balestiki ambayo yanatwajwa kuwa ya masafa marefu yenye uwezo wa kupaa kutoka bara moja hadi jingine.

Gazeti hilo lilifafanuwa kuwa, makachero wa Marekani na Korea Kusini wamenasa taarifa za kiintelijensia zinazoonyesha kuwa, Korea Kaskazini imefanikiwa kutengeza na kukamilisha uundaji wa makombora hayo katika kiwanda kimoja cha utengezaji makombora kilichopo mjini Shinpo katika Jimbo la Kusini la Hamgyong. Zaidi soma Gazeti la Majira popote ulipo Tanzania