Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Waziri wa Uchukuzi
David Kihenzile (Mb) akipata maelezo kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa
Bodi ya Wakurugenzi TCAA Bi. Mtumwa Ameir alipotembelea banda la
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) na kupata maelezo kuhusu
utendaji wa shughuli za Mamlaka pamoja na Chuo cha Usafiri wa Anga
Tanzania (CATC) katika maonesho ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya
miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanayofanyika katika viwanja vya Fumba, Zanzibar.

Kihenzile ameipongeza TCAA kwa usimamizi mzuri wa Sekta ya Usafiri wa Anga na kuahidi serikali itaendelea kuwekeza katika sekta hii muhimu pia alisisitiza chuo kuendelea kujitangaza zaidi ili kisikike na kuwafikia watu wengi Zaidi ndani na nje ya nchi.


More Stories
Rais Samia amrudisha January kwa Mama,asema kilichotokea ni kumuonya
Milioni 236 kunufaisha vikundi 17 vya wanawake Minazi Mirefu
Mipango 10 kabambe ya TPA