October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally Kakurwa mara baada ya Mgombea Urais wa CCM kwa upande wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi kusimama mbele ya Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM NEC kwa ajili ya kuwasalimia.

Kauli ya Dkt. Mwinyi baada ya kuchaguliwa

Na David John, TimesMajira Online

WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa wamemchagua Dkt Hussein Mwinyi kuwa mgombea Urais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika uchaguzi unatarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

Dkt.Mwinyi ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi amechaguliwa kwa Kura 129 sawa na asilimia 78.65%, katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete wa White House Makao Makuu ya nchi Dodoma.

Mkutano huo ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli na Makamu Mwenyekiti Zanzibari na Rais wa Serikali ya Mapinduzi, Dkt Mohamed Shein, Makamu Mwenyekiti Bara, Philip Mangula, Katibu Mkuu wa Chama hicho Dkt Bashir Ally na viongozi wengine waandamizi wa CCM .

Baada ya kuchaguliwa Dkt Mwinyi alonga.

Mgombea Urais kwa Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM kwa upande wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi akizungumza kuwashukuru Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM NEC mara baada ya kuchaguliwa katika mkutano huo uliofanyika katika Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma.

Akizungumza mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu Dkt Hussein Mwinyi alianza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwani kazi hiyo haikuwa rahisi.

“Msionione nimepungua, kazi hii hakuwa rahisi hivyo namshukuru Mungu na ninyi wajumbe wa mkutano mkubwa kwa imani kubwa mlioonyesha kwangu “amesema Mwinyi .

Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu wa Chama cha Mapinduzi CCM NEC wakishangilia wakati Kikao cha NEC kikiendelea katika Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma.

Dkt Mwinyi amebainisha kuwa kura 129 ni kura nyingi sana na kwamba wajumbe wa mkutano mkuu wameonyesha kuwa na imani naye na hakuna shaka kwamba atalitumikia taifa kwa uwezo wake wote.

Amefafanua kuwa atakuwa tayari kushirikiana na wezake wote na kwamba baada ya kumalizika kwa mchakato huo hivi sasa timu ni moja tu na so zaidi ya hapo.

“Nitashirikiana na viongozi wote wakiwamo wale ambao wameingia kwenye tano bora, hadi tatu wote kwa ujumla tutakuwa pamoja,” amesema Dkt Mwinyi 

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na kuwashukuru Wajumbe wa NEC katika Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma.

Mteule huyo ambaye anakwenda kupeperusha bendera ya CCM kwa nafasi ya urais Zanzibar aliwaeleza wajumbe hao kuwa amefanya kazi na mitihani mingi lakini mtihani mkubwa ulikuwa ni wakinyang’anyilo hicho na anaamini kazi hiyo itakuwa sio ya peke yake bali ni ya wote.

“Mungu awabariki sana.” Alimaliza Dkt Mwinyi.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza na Wajumbe wa NEC mara baada ya kumpata Mgombea Urais wa CCM upande wa Zanzibar katika kikao cha NEC kilichofanyika White House jijini Dodoma. PICHA NA IKULU