Na Mwandishi Wetu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ameongoza kikao cha Jimbo la Serikali kilichofanyika Agosti 24,mwaka huu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Serengeti uliopo Jengo la Ushindani Dar es Salaam.
Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania(TACAIDS) pamoja na Bohari ya Dawa (MSD).

Kikao hicho kililenga kujadili utekelezaji wa Programu za Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu, na Uimarishaji wa Mifumo ya Utoaji Huduma za Afya nchini kupitia ufadhili wa Mfuko wa Dunia (Global Fund).
Aidha, kikao hicho ni sehemu ya maandalizi ya kikao cha Tanzania National Coordinating Mechanism (TNCM) ambacho wajumbe wake ni Jimbo la Serikali, Asasi za Kiraia (NSA), na Wadau wa Maendeleo.
More Stories
Ofisi ya Msajili Hazina yaendesha mafunzo kwa kamati za bunge
Dkt Biteko awataka Watanzania kumuenzi hayati Baba wa Taifa
Dkt.Yonazi akutana na kufanya mazungumzo na mtakwimu Mkuu wa Serikali