*Ni katika majimbo ya Kibamba na Ubungo
*Kairuki aishukuru Halmashauri Kuu ya CCM
Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online-Dar
Angela Kairuki amechuku fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Kibamba huku Kitila Mkumbo akichukua fomu kwa ajili ya Jimbo la Ubungo,ambapo wote wawili wakipeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).
Fomu hizo zimetolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi(INEC),kupitia Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kibamba na Ubungo Rosemary Mpeleta katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo,Agosti 25,2025.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo,Angela Kairuki, ameishukuru Halmashauri Kuu CCM Taifa kwa kumteua kupeperusha bendera ya chama hicho Jimbo la Kibamba.
Kairuki amesema yupo tayari kuwatumikia wananchi wa Kibamba bila kujali itikadi kwa kuleta maendeleo na fursa mbalimbali ili kukuza uchumi wa Jimbo hilo.
Kwa upande wake Kitila Mkumbo,amewaomba wananchi wa Ubungo kujitokeza kwa wingi Agosti 28,2025, Tanganyika Parks katika uzinduzi wa kampeni za CCM kitaifa.
Mbali na hao mgombea Udiwani wa CCM Kata ya Mbagala wilayani Temeke Abdulkarimu Pazi,amesema atakaposhinda nafasi ya Udiwani atazingatia utu bila upendeleo kwani chama hicho kinategemewa na wananchi pamoja na nchi.


More Stories
Wanawake washauriwa kuchangamkia fursa za uchumi
Aida:Wanawake wakipata haki zote itapunguza migogoro
LGTI wanawake waadhimisha siku yao Ngorongoro