Na Moses Ng’wat, TimesMajira Online, Mbozi.
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mlowo, Wilayani Mbozi, Misheck Mwambogolo, (47) amejinyonga hadi kufa kwa kutumia kamba ya manila shambani kwake .
Mwambogolo ambaye pia ni Katibu wa Chama cha Msingi cha ushrika (Amcos) cha Shimondo, Wilayani hapa, anadaiwa kujinyonga kutokana na masuala ya biashara ya Kahawa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Theopista Mallya, akizungumzia tukio hilo leo Jumatatu, Aprili 24, 203 amesema lilitokea saa 7:00 usiku baada ya kukutwa akiwa amejinyony
onga juu ya mti kwa kutumia kamba ya manila.

Kamanda Mallya amesema marehemu aliacha ujumbe wa maandishi kwenye gari yake, kama unavyosomeka kwenye taarifa ya jeshi hilo la polisi Mkoa wa Songwe.
More Stories
TFS yawakaribisha wawekezaji katika vivutio vya utalii wa misitu
Waziri Bashungwa:Tumieni teknolojia za kisasa kudhibiti uhalifu unaovuka mipaka
Flightlink kuzindua Safari za Ndege za Kila Siku kwenda Nairobi wiki ijayo