Na Mwandishi Wetu, Timesmajira
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino amechaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho hilo kwa muda wa miaka mingine minne kuanzia 2023 hadi 2027
Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo uliofanyika mjini Kigali, Rwanda Infantino amesema kuwa Rais wa FIFA ni heshima kubwa na furaha lakini ni jukumu kubwa pia.
“Kuwa Rais wa FIFA ni heshima kubwa, ni fursa ya ajabu. Pia ni jukumu kubwa. Hakika nimeguswa na sapoti yenu. Nawaahidi nitaendelea kuitumikia FIFA, kutumikia mpira wa miguu duniani kote, kutumikia vyama vyote 211 vya FIFA,” amesema Infantino.
More Stories
Kasulu FC mabingwa mashindano Khimji 2025
Fainali Khimji cup kufanyika Februari 7,2025
Naibu Waziri wa Fedha abariki ujio mpya wa Bahati Nasibu