Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MAOFISA wa Jeshi la Polisi 155 waliopandishwa vyeo na Rais Samia Suluhu Hassan, wamekula kiapo cha utii kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi na kiapo cha maadili ya viongozi wa umma.
Maofisa hao ambao ni makamishna wasaidizi waandamizi wa Polisi, wapo 27 waliopanda vyeo kuwa manaibu kamishna.
Pia wamo makamishna wasaidizi wa Polisi ambao wamekuwa makamishna wasaidizi waandamizi wa Polisi, ambao ni 128.

Akitoa nasaha Februari 19, 2024 Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camillus Wambura amesema, kupandishwa vyeo kwa maofisa hao, kutaongeza chachu ya utendaji kazi, kutenda haki, uadilifu na nidhamu pia wananchi wategemee mabadiliko makubwa ya kiutendaji.
Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, CP Susan Kaganda amesema miongoni mwa waliopandishwa vyeo, wapo maofisa wanane wa kike, ambao wamepanda vyeo na kuwa manaibu kamishna wa Polisi.
Akizungumza kwa niaba ya waliopandishwa vyeo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi David Misime amesema kupanda kwao vyeo, kutaongeza morali na utimamu zaidi wa akili katika kutekeleza majukumu ya kazi za Polisi.
More Stories
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka