Na Mary Margwe, Timesmajira Online,Bahati
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga,amesema kwa mara ya kwanza Mkoa huo utaanza kutoa huduma ya kusafisha Figo(dialysis).
Sendiga ameyasema hayo Februari 6, 2025 wakati akizindua rasmi Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara,ambapo ameeleza kuwa huduma ya usafishaji wa figo itatolewa ndani ya siku 5-6 kuanzia Februari 6, 2025, na hivyo kuwata wananchi kutumia siku hizo kwa ajili kupata huduma hiyo.
Ambapo Mkoa wa Manyara,umepata mashine 6 za usafishaji wa figo kwa ajili ya kutoa huduma hiyo, zitakua na uwezo wa kusafisha damu za wagonjwa 12 kwa siku, ambapo zitasaidia kupunguza adha, gharama na muda kwa wagonjwa ambao wamekua wakifuata huduma hiyo mbali ukilingamisha na Sasa itakua ikipatikana ndani ya Mkoa husika.
Sendiga ameiwaasa bodi hiyo akiwemo Mwenyekiti na wajumbe,kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa uadilifu, uwazi na kwa kuzingatia maslahi ya jamii
na si vinginevyo
Aidha amesema kazi kubwa ya bodi hiyo ni kushauri uongozi wa hospitali, kusimamia huduma bora kwa wananchi pamoja na matumizi sahahi ya rasilimali zilizopo hospitalini hapo.
More Stories
Ofisi ya Msajili Hazina yaendesha mafunzo kwa kamati za bunge
Dkt Biteko awataka Watanzania kumuenzi hayati Baba wa Taifa
Dkt.Yonazi akutana na kufanya mazungumzo na mtakwimu Mkuu wa Serikali