Viongozi wa Jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Magharibi ECOWAS wamekutana hii leo kujadili mapinduzi ya kijeshi nchini Mali, yaliyomuondoa madarakani rais Ibrahim Boubacar Keita.Â
Ni Kwa muda mrefu jumuiya hiyo imekuwa ikijaribu kusuluhisha mgogoro huo kabla ya mapinduzi ya Jumanne wiki hii.Â
Akizungumza Afisa wa jeshi la nchi hiyo  kanali Assimi Goita ametangaza jana kuwa ndiye kiongozi wa mapinduzi nchini humo.
Umoja wa Afrika tayari umeisimamisha Mali kufuatia mapinduzi ya Jumanne, na kuungana na jumuiya nyingine za kimataifa ikiwemo Umoja wa Mataifa na ule wa Ulaya kulaani vikali mapinduzi hayo.
Kundi la mataifa matano ya kanda ya Sahel limewataka wanajeshi walioongoza mapinduzi kumuachia rais Keita na maafisa wengine wa serikali yake wanaowashikilia.

More Stories
Migogoro na uhamishaji  janga lakisiasa, kibinadamu barani Afrika
Wanasayansi Wafichua siri nzito kuhusu chanzo cha viazi vya chips
Gavu asisitiza kuimarisha ushirikiano Tanzania na China