Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MSANII wa muziki wa Bongo fleva na Bosi wa Wasafi Media Naseeb Abdul maarufu ‘Diamond Platnumz’, leo ameachia wimbo mpya ujulikanao ‘Waah!’ aliomshirikisha mkongwe wa muziki wa dansi kutoka nchini Congo Koffi Olomide.
Wimbo huo umeachiwa katika ofisi za Makao Makuu ya Wasafi Media ambapo Koffi Olomide amepata nafasi ya kuangalia namna ya utendaji na uzalishaji wa vipindi unavyofanyika katika Media hiyo akiongozana na mwenyeji wake Diamond Platnumz.
Hata hivyo, Koffi amesifia namna ambavyo kuna mipango kazi mizuri ndani ya Wasafi Media, lakini pia akimpongeza Diamondplatnumz kwa kuweza kutoa nafasi ya ajira kwa vijana zaidi.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”