Na Heri Shaaban,Timesmajiraonline,Ubungo
MKUU wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando,amesema mikakati yake katika wilaya ya Ubungo ni kuitambua sekta isiyo rasmi ya Waendesha Pikipiki maarufu bodaboda kwa kuwasajili kuwapatia vyeti vya kuzaliwa na vitamburisho vya Taifa NIDA ili waweze kupewa leseni za udereva waweze kumiliki Pikipiki zao.
Msando amesema hayo jijini hapa leo Mei 29,2025 wakati akizungumza kwenye mkutano wa vyama vya Ushirika Mkoa Dar Es Salaam.
“Mikakati yangu mwezi huu tunatarajia kuwasajili waendesha bodaboda wa Ubungo wote waweze kupata vyeti vya kuzaliwa watengeze NIDA yao waweze kupata leseni wamiliki Pikipiki zao watoke katika biashara ya kuajiliwa kwa mkataba inawanyonya,”amesema Msando.

Amesema anatoa maelekezo hayo kwa watendaji wake wa wilaya ya ubungo waanze kutekeleza mara moja ili vijana wa bodoboda wapate fursa hii haraka wakuze uchumi ushirika wao ukue.
Alisema waendesha bodaboda wa Ubungo kupitia ushirika huo wakiwa na NIDA, TRA na vyeti vyao vya kuzaliwa ni Rais kutambulika waweze kukopa mikopo ya ushirika au mikopo ya Serikali kwa kuwa wanatamburika rasmi
Amesema sekta hiyo isiyo rasmi ya bodaboda wanafanya kazi ngumu wengi wao hawana leseni hivyo wanafanya kazi kutegemea mikataba ya unyanyaaaji kutoka kwa mabosi wao.
Aliwataka maafisa maendeleo wa kata Ubungo na Maafisa watendaji kata jukumu lao kwa sasa kuwatambua vijana hao ambao ni watu muhimu na wana mchango mkubwa kwa jamii na Serikali.
Alitoa agizo kwa vyama vya ushirika kuwatumia bodaboda ni watu muhimu katika sekta ya kukuza uchumi wa nchi yetu hivyo wana ushirika kuwatumia vizuri kuwapa elimu waweze kutekeleza majukumu yao kwani vijana wengi wa bodaboda asilimia 93 wanalipwa shilingi 300,000 ila hawana mikopo ya Serikali .
Akizungumzia sekta ushirika alisema alitoa wito kusimamia vyema sekta ya ushirika na kuzitaka kampuni za simu zisiwabane wana ushirika kutokana na mikopo hiyo kutokana na riba zao katika utekelezaji wa majukumu yao
Alivitaka vyama vya ushirika mkoa wa Dar es salaam kusimamia vyema sekta ya ushirika na kuzitaka kampuni za simu zitekeleze majukumu yao ya simu waache mambo ya songesha na kuwadai pesa wananchi.
Aidha aliagiza matumizi ya Mfumo wa Digitali TEHAMA utumike kwa vyama ushirika vyote kwani Dunia kwa sasa ipo katika mfumo huo .

Alizitaka kampuni za simu zisiwabane wana ushirika kupitia mikopo ya simu za mkononi kutokana na kuwepo kwa riba kubwa .
Katika hatua nyingine amevitaka vyama vya ushirika visibague vyama vya chini kutokana na mitaji yao kuwa midogo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Dar es Salaam,Enerest Nyambo, amesema kuwa jukwaa hilo ni la nane kufanyika na lina lengo la kutoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili waajiri na waajiriwa katika maeneo yao ya kazi.
“Tuna ufadhili kutoka taasisi mbalimbali za kifedha kupitia jukwaa hili, tunapokea maelekezo ya viongozi wa serikali na kuyatekeleza kwa wakati.
Nyambo alisema wanahimiza wanachama wa vyama vya ushirika kufuata taratibu zote zinazohusu utoaji wa mikopo
Pia alisema Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika mkoa wa Dar es Salaam, limelenga kuweka mikakati ya pamoja ili kuboresha huduma kwa wanachama na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia ushirika.


More Stories
AI Spam Filter na Usalama wa Data Zako
Bodi ya Ithibati yasisitiza Waandishi wa Habari kuweka vyeti vya kitaaluma katika mfumo wa Tai-Habari
REA yahamasisha wananchi kutumia Mkaa Mbadala