Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imefungua dawati la huduma kwa wateja kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma juu ya huduma mbalimbali za Mamlaka ikiwemo utaratibu wa upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Kata ya Majohe, Wilaya ya Ilala ambao ni sehemu ya wanufaika wa utekelezaji wa mradi wa maji Majohe.

Utekelezaji wa mradi wa maji Majohe umehusisha ulazaji wa mabomba ya inchi 8,6,4 na 3 kwa umbali wa kilomita 46 na utahudumia wananchi takriban 24,000.

More Stories
Milioni 299 kutumika kujenga ofisi za kata
Mtanda asisitiza matumizi ya takwimu serikalini
Maofisa Habari watakiwa kuhabarisha taarifa sahihi