May 17, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Fursa kwa wakulima na wafannyabiashara zatanganzwa

Na Mwandishi wetu.Iringa.

MWENYEKITI wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) Salum Awadh ametangaza fursa mbalimbali zinazotolewa na CPB kwa wakulima na wafanyabiashara wa Mazao hapa nchini.

Aidha Awadh ametaja baadhi ya fursa zinazotolewa na CPB ni pamoja kilimo cha mkataba ambacho kitaanzia na hekali 1000 na kuendelea.

Akizungumza katika kikao cha wadau kilichofanyika leo Iringa, Awadh amesema Kilimo cha mkataba CPB kitakuwa na uwezo mkubwa kutoa maelekezo na ufuatiliaji kwa urahisi.

” Kilimo cha mkataba kitasaidia kuwa na uhakika wa wakulima watakaotuletea mazao, yatakuwa katika ubora”‘ amesema Awadh.

Mwenyekiti huyo amesema fursa zingine ni pamoja na kuhitaji Mawakala ambao wataingia nao mkataba kwaajili ya uuzaji wa bidhaa zinazozalishwa CPB na kununua mazao kutoka kwa wakulima na wafanyabishara.

Awadh amesema CPB ni Shirika la Kibiashara la Serikali hivyo linafanya biashara kwa lengo la kuinua Uchumi wa Nchi lakini na mtu mmoja mmoja.

“Biashara ambayo CPB inafanya hatuwezi kumlalia mkulima au mfanyabiashara wa mazao, Sisi lengo letu, Sisi tupate na nyie mpate,amesema Mwenyekiti huyo wa Bodi.

Aidha Awadh amesema CPB ina maghala ambayo hutumia kuhifadhia mazao na bidhaa zao, hivyo wanafanya pia biashara ya kuhifadhi mazao katika maghala hayo ambayo yapo katika Mikoa mbalimbali.

vilevile Mwenyekiti huyo amesema kuwa CPB pia inatafuta masoko kwa Wakulima kama wanunuaji lakini kuwatafutia wakulima na wafanyabiashara kuwa inganisha na masoko ya nje.

Aidha Awadh amesema CPB inaongezea thamani mazao kwa kuchakata mazao kama Mpunga, Mahindi, Ngano, Alizeti na Siagi kupitia Viwanda vya CPB vilivyopo katika baadhi ya Mikoa ikiwemo Iringa hivyo wafanyabiashara na wakulima wa mazao watumie fursa hiyo ili kuinua uchumi wao.

Aidha Mwenyekiti huyo amesema katika kujiimarisha katika uchakataji wa mazao wanatarajia kujenga viwanda vingi zaidi katika Mikoa mbalimbali.

Awadh ametaja mikoa ambayo tayari kuna viwanda vya kuchakata mazao kuwa ni , Dodoma ambapo kuna kiwanda cha kuchakata Mahindi na Alizeti.

Ametaja Mikoa mingine kuwa Arusha kuna kiwanda cha kuchakata Mahindi na Ngano, Iringa kiwanda cha kuchakata Mahindi, Mwanza kiwanda cha kuchakata Mpunga na Dar eslaam kuna Kiwanda cha kuchakata Siagi ya Korosho.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Elia Luvanda ambaye alifungua kikao hicho ameitaka CPB kuangalia uwezekano wa kujenga kiwanda cha unga wa lishe kwaajili ya wanafunzi mashuleni.

“Unajua ukanda huu wa Nyanda za juu kuna tatizo la watoto kukosa lishe,hivyo niwaombe CPB mbali na kufanya biashara ya mazao,wajenge kiwanda cha kutengeneza lishe ili watoto wetu waondokane na utapiamlo’, amesema Luvanda.