Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MUIGIZAJI mahiri kutoka nchini Afrika Kusini, Connie Chiume ambaye pia ni Muigizaji wa Filamu ya Black Panther, ametoa mafunzo maalum kwa wasanii yaliyoratibiwa na Taasisi ya Refocus Africa kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu Tanzania.
Mafunzo hayo ya ubobevu (master class) yalilenga kuimarisha uwezo wa Waigizaji kwenye maeneo ya uigizaji, namna ya kutambua kipaji, kuthamini kazi ya Sanaa kwa Muigizaji, ikiwemo nidhamu, pamoja na ushirikiano wa kimataifa katika filamu.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo pamoja na Balozi wa Bodi ya Filamu, Muigizaji Yvonne Cherrie almaarufu Monalisa, waliungana na Wanatasnia ya Filamu katika mafunzo hayo.
More Stories
Tamasha la utamaduni mkoani Ruvuma lapamba moto, Rais Samia mgeni rasmi
TANAPA yazindua Twenzetu Kilele msimu wa nne
Shamrashamra maadhimisho ya miaka 60 JWTZ yaendelea