Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MUIGIZAJI mahiri kutoka nchini Afrika Kusini, Connie Chiume ambaye pia ni Muigizaji wa Filamu ya Black Panther, ametoa mafunzo maalum kwa wasanii yaliyoratibiwa na Taasisi ya Refocus Africa kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu Tanzania.
Mafunzo hayo ya ubobevu (master class) yalilenga kuimarisha uwezo wa Waigizaji kwenye maeneo ya uigizaji, namna ya kutambua kipaji, kuthamini kazi ya Sanaa kwa Muigizaji, ikiwemo nidhamu, pamoja na ushirikiano wa kimataifa katika filamu.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo pamoja na Balozi wa Bodi ya Filamu, Muigizaji Yvonne Cherrie almaarufu Monalisa, waliungana na Wanatasnia ya Filamu katika mafunzo hayo.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”