June 6, 2025

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Coca-Cola Kwanza kuwanufaisha mama lishe Stendi ya Msamvu Marogoro

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online

KATIKA kuhakikisha wanawake wajasiriamali na Mama Lishe wanapata huduma iliyo bora mkoa Morogoro, Kampuni ya Coca-Cola Kwanza imekabidhiwa eneo maalumu katika Stendi ya Msamvu kwa ajili ujenzi wa soko mkoani humo.

Hafla ya makabidhiano ya eneo hilo maalumu kwa ajili ya soko ilifanyika katika ofisi za Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro.

Katika tukio hilo Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,Emmanuel Mkongwa alikabidhi rasmi eneo hilo kwa kampuni hiyo ya Coca-Cola Kwanza kwa ajili ya kuanza ujenzi wa soko maalum.

Mradi huo ni sehemu ya juhudi za kampuni hiyo kuimarisha wanawake wajasiriamali na kuchangia maendeleo ya kijamii katika Manispaa ya Morogoro.

Katika hafla hiyo, pia walihudhuria maafisa waandamizi kutoka Manispaa ya Morogoro pamoja na wawakilishi wa Coca-Cola Kwanza.

Afisa Uhusiano na Mawasiliano ya Umma wa Coca-Cola Kwanza, Maria Kimwaga (wa pili kutoka kushoto), akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Emmanuel Mkongwa (wa pili kutoka kulia), katika hafla rasmi ya makabidhiano ya eneo la Stendi ya Msamvu kwa Kampuni hiyo.