Na Mwandishi wetu,Timesmajira
KADA wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Rorya ambaye aliyewahi kuwa mtumishi wa CCM Makao Makuu Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Baraka Otieno, ametoa rai kwa Kamati ndogo ya Udhibiti nidhamu inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Steven Wassira kuunda timu maalum ya kuchunguza vitendo vinavyofanywa na Mwenyekiti wa Wilaya ya Rorya Ongujo Wakibara cha kuwagawa Viongozi wa Chama na Watendaji.
Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kada huyo amesema Mwenyekiti huyo
amekuwa akiwatishia wajumbe na madiwani kuwa atakata majina yao kama hawatamuunga mkono Mbunge wa sasa wa Jimbo hilo Jafari Chenge.
Amesema Mwenyekiti na Mbunge huyo wamekuwa na tabia ya kuwagawa na kuwabagua viongozi wa Kata na Matawi ambao hawapo katika mlengwa wao jambo ambalo halina afya kwa Chama.
“Viongozi wengi wanaobaguliwa na Mwenyekiti huyo ni wale wanaotoka katika tarafa ya Dirango na baadhi ya kata ya Zuloimbo na Suba.
Amesema Mwenyekiti huyo amekuwa akiagiza viongozi wa chama ngazi ya kata kuwasimamisha viongozi bila kufata katiba wala kanuni za maadili wala kuhusisha kamati ya siasa ya wilaya.
“Tunayazugumza mambo haya ili wanaccm nchi nzima waelewe kinachoendelea wilayani Rorya, kamwe hatuwezi kunyamazia vitendo kama hivi vinavyofanywa na Mwenyekiti huyu kwani
imefika mahali rorya wanaccm na wananchi kwa ujumla wanajiuliza Chama hiki kimetekwa na wafanyabiashara kiasi cha kufanya matukio ya utovu wa nidhamu na wasichukuliwe hatua,”amesema Otieno
Aidha amesema wananchi wa Wilaya ya Rorya wanaonesha dhahiri kukichoka chama cha mapinduzi kwasababu ya Ongujo,kutokana na fedha zake anafanya kama anaimiliki CCM,kwani hadi baadhi ya vikao vya CCM ngazi ya Wilaya vinafanyika nyumbani kwake.
”Mwenyekiti huyu anatawaliwa na ubinafsi,CCM ndani ya wilaya ya Rorya ipo kwenye wakati mgumu sana kutokana na ubinafsi huo uliopitiliza wa mwenyekiti huyo anayewagawa wanaccm katika mafungu kutokana na ubinafsi huo.
Amesema kuhusu ukweli,Mwalimu Nyerere aliwahi kusema ukweli una tabia moja nzuri haujali mkubwa wala mdogo,adui au rafiki kwake watu wote ni sawa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Ongujo Wakibara, amesema hali ya kisiasa ndani ya wilaya hiyo iko shwari japokuwa lipo vuguvugu linalosababishwa na wakati uliopo wa kuelekea uchaguzi mkuu ambao utafanyika baadaye mwaka huu.
Hata hivyo, Wakibara amesema Chama kimesimama imara kuwaunganisha wanachama wote huku pia kikiwalinda viongozi wawakilishi wa wananchi wamalize kipindi chao cha uongozi na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025.
“Mimi nikiwa msimamizi mkuu wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika eneo langu naendelea kuwalinda viongozi wa kuchaguliwa akiwemo mbunge, madiwani na viongozi wa serikali za mitaa wanaotokana na Chama chetu,” amesema.
Pamoja na kuhakikisha viongozi hao wanapewa nafasi ya kuwatumikia wananchi, pia wanachama wote wa CCM wameendelea kupewa fursa ya kukitumikia Chama na muda utakapowadia kila mmoja atapata fursa ya kupambania nafasi za uongozi.
“Kwa sasa tunaowatambua wanatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ni mbunge (Jafari Chege), madiwa na viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji, tuwape nafasi wakamilishe ngwe yao katika utekelezaji wa ilani,” amesema.
More Stories
KNOCK OUT ya Mama Msimu wa tatu kufanyika Februari 28
Rais Samia ataka watumishi kumaliza adha ya maji kwa wananchi
Serikali, wadau waombwa kusapoti mashindano ya Lina PG Tour