Na Iddy Lugendo, Timesmajira Online
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania katika Maonesho ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya Bombambili, halmashauri ya mji wa Geita.
Kigahe amefahamishwa kuwa pamoja na jitihada zingine katika kuhakikisha nchi inakuwa na akiba ya kutosha ya fedha za kigeni, Benki Kuu imeanza kununua dhahabu ghafi kutoka kwa Wachimbaji wakubwa, wadogo na wa kati.
Maonyesho hayo ambayo hufanyika kila mwaka, yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 23, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko na yatafikia kilele Septemba 30, 2023 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi siku ya kufunga maonesho hayo.
Maonesho hayo yenye kauli mbiu; Matumizi ya teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi mazingira yamewaleta pamoja washiriki zaidi ya 400.
More Stories
Wanachi wahimizwa kusajili biashara,majina ya kampuni BRELA
Bunge lapitisha muswada wa Sheria za kazi,wanaojifungua watoto njiti waongezwa likizo ya uzazi
GreenFaith yatoa mapendekezo yake mkutano wa mission 300 kwa Wakuu wa nchi,Serikali za Afrika