Na Penina Malundo,Timesmajira
Waziri Mkuu wa Mstaafu wa Ethiopia na Mratibu Mwenza wa Jukwaa la nane la Kikanda la Viongozi Afrika (ALF), Hailemariam Desalegn Boshe amesema wamekutana katika Jukwaa hilo kwa jambo la kutambua maendeleo endelevu ya Bara la afrika.
Ameyasema hayo leo Kampala ,Uganda katika Kongamano la nane la Kikanda la Viongozi Afrika (ALF) lililoanza leo na kumalizia Aprili 8 mwaka huu lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi.

Amesema miongoni mwa mpango wa SDGs kipengele cha 17 kinawakilisha mpango bora wa maisha yajayo na hamu ya pamoja ya kuondokana na umaskini,kutokuwa na usawa na uharibifu wa mazingira.

“Ni wakati wa kutumia teknolojia za kidijitali na kukuza uvumbuzi kunaweza kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha utoaji wa huduma,” amesema.

More Stories
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako
TTCL yaadhimisha siku ya Wanawake kwa kutoa msaada JKCI
Wananchi Dodoma washauri TBA kujenga nyumba za kupangisha watu binafsi