Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Uwakilishi wa Benki ya NMB ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Bi. Ruth Zaipuna umehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Huduma za Kijamii ya Kikristo (CSSC), mkutano unaoangazia masuala ya elimu na afya. Mkutano huu unafanyika jijini Dar es Salaam kwa siku mbili.
Benki ya NMB imekuwa na ushirikiano mzuri na Kamisheni hii ambapo baadhi ya mashule na hospitali zao zimekuwa zikitumia mifumo ya Benki ya NMB ya kidijitali inayorahisisha ukusanyaji wa Sadaka, ulipaji bili za huduma za afya na uchangiaji wa miradi mbalimbali. Zaidi, mifumo hii imesaidia kupunguza upotevu wa mapato, kupunguza gharama kubwa za uendeshaji, kuonyesha uwazi, usimamizi wa miamala (yaani reconciliation) na kufanya malipo mbalimbali kwa wakati.
Mkutano huu umeongonzwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kamisheni ya Huduma za Kijamii ya Kikristo, Ndg. Peter Maduki na kuhudhuriwa na Maaskofu wote nchini.
NMBKaribuYako



More Stories
Visima 67,000 vya umwagiliaji kuchimbwa nchiniÂ
DC Songea ahimiza matumizi na uwekezaji kwenye nishati safi
PPPC yawanoa wabunge umuhimu wa utaratibu wa PPP kwenye miradi