Na Jackline Martin, TimesMajira Online
Benki ya –KCB imetia saini mkataba wa makubaliano –MOU na Benki ya uwekezaji ya umoja wa Ulaya –EU, wa mkopo wenye thamani ya shilingi bilioni 50 kwa lengo la kuwawezesha wajasiriamali wanawake Nchini.
Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, Mkurugenzi wa –KCB, Cosmas Kimario amesema mkataba huo umechangiwa na mazingira wezeshi yanayofanywa na Serikali chini ya Rais Dkt Samia Suluhu.
“Mkataba tuliousaini na Europian wa mkopo wa Euro milioni 20 ambao ni takribani bilioni 50 za kitanzania utakwenda kuwasaidia wakina mama katika harakati zao za ujarisiliamali.”

Amesema ni wazi kuwa sekta ya ujasiriamali Nchini inahusisha wanawake wengi zaidi Nchini hivyo –KCB itaendelea kuleta huduma bunifu zitakazomlenga mtanzania moja kwa moja.

Pia ameishukuru serikali kwa kuendelea kuiunga mkono sekta binafsi na kutengeneza mazingira ambayo yanawafanya wawekezaji wa nje kuongeza na kuja kuwekeza nchini.
Itakumbukwa kuwa serikali imeendelea kuhamasisha taasisi za fedha Nchini kuunga mkono jitihada za serikali katika kuwainua wajasiriamali nchini wakiwemo wanawake ambapo –KCB imetekeleza hilo.
More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo