Na Esther Macha Timesmajira Online, Mbeya
Askari waJesho la Polisi Mkoa wa Mbeya J. 2596 Kostebo Samweli Kaziyote (24) wa kituo kikuu cha polisi Mbeya anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi kidevuni na kusababisha kifo chake.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema kuwa tukio hilo limetokea Octoba 2 mwaka huu majira ya saa 2.15 usiku huko maeneo ya mtaa wa Mzumbe Forest ya zamani.
Kamanda Kuzaga amesema kuwa askari huyo alijipiga risasi kidevuni na kusababisha kifo chake hapo hapo
Hata hivyo Kamanda Kuzaga amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni mzozo uliotokea baina yake na mpenzi wake baada ya marehemu kuacha lindo la benki kisha kuondoka na silaha hiyo kwenda nyumbani kwa mpenzi wake huyo na kujipiga risasi.
Hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.
More Stories
Rais Mwinyi aipongeza Kampuni ya Yas kushirikiana na ZHC
Raha ya WiFi za bure na mtego kwa taarifa zako za siri
Mke wa Rais wa Finland atembelea Makumbusho ya Taifa