Na Rose Itono,Timesmajira
Airtel Tanzania Leo Juni 13 imeungama na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ( NEMC) kufanya usafi kwenye fukwe ya Bahari ya Kidimbwi maarufu Beach Kidimbwi’ iliyopo Kata ya Kawe Mtaa wa Mbezi Beacha B Dar es Salaam ili kutokomeza taka za plastiki
Pia Airtel imekabidhi vifaa Vya usafi kwa Uongozi wa Mtaa wa Mbezi Beach B ili kuendeleza usafi na kufanya mazingira yabaki salama
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mara baada ya zoezi la usafi kumalizika Kaimu Meneja wa Mazingira Kanda Ya Mashariki Kaskazini
Pia Airtel inaungana na serikali katika mkakati wake wa kuweka.mazingira safi na kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki kwa Kauli mbiu ya Pamoja tutokomeze taka za plastiki

” Leo tumeungana na NEMC, Halmashauri ya Kinondoni,viongozi wa Mtaa wa Mbezi Beach B na wananchi wake kufanya usafi ufukwe wa Kidimbwi maarufu ‘ Beach Kidimbwi’ ili kutokomeza taka za plastiki ambazo zinachangia kuharibu mazingira na kuzuru viumbe wa bahari,” amesema Singano
Aidha amewataka wananchi kubadili tabia na kupunguza taka za plastiki ili kulinda viumbe wa bahari ambao wanachangia ukuaji wa uchumi wa nchi
Amesema Airtel itaangalia namna ya kuweka utaratibu wa kudumu kuhakikisha wanajipanga kufanya usafi kwenye fukwe ili ziweze kubaki salama

Kwa upande wake Afisa Mazingira Mwandamizi akimwakilisha Kaimu Meneja wa Mazingira Kanda Ya Mashariki Kaskazini Jeremia Nyakwaka amewataka watanzania kulinda na kuhifadhi mazingira ya fukwe ili yaweze kubaki salama
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mbezi Beach B Asha Vionatis ameishukuru Airtel kuungana na wananchi wa mtaa wake kufanya usafi kwenye fukwe hiyo na kuomba zoezi hili liwe endelevu ili kulinda Mazingira ya fukwe sambamba na kuyaweka yabaki salama kwa viumbe Vya makini na jamii pia
Hata hivyo ameshukuru kwa vifaa vilivyotolewa kwa ajili ya kuendeleza usafi katika Mtaa huo huku akiahidi kushirikiana na wananchi wake kuhakikisha fukwe na.mtaa wao kwa ujumla.unakuwa wa kuigwa kwa suala la usafi
More Stories
Waziri Mkuu kuzindua Kampeni ya msaada wa kisheria Dar
Bilioni 190 kuimarisha mafunzo ya ufundi stadi
Makongoro aielekeza Halmashauri ya Nkasi hoja za kufanyiwa kazi haraka