Na Mwandishi wetu,Timesmajira
Airtel Tanzania, kupitia kikundi cha wafanyakazi wanawake kinachojulikana kama Airtel Divas, kimetoa msaada muhimu kwa wagonjwa wa saratani ya matiti katika Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) kwa kulipia gharama za kliniki kwa zaidi ya wagonjwa 40 waliokuwa hawawezi kumudu gharama za kuendelea na kliniki ya afya baada ya matibabu.
Kufanya wa klinniki ni sehemu muhimu ya matibabu baada ya saratani, kwani husaidia kufuatilia afya ya mgonjwa, kugundua mapema changamoto yoyote, na kuhakikisha marejeleo ya afya ya muda mrefu.
Hata hivyo, baadhi ya wanawake waliohitimisha matibabu yao walikuwa wameshindwa kuhudhuria ukaguzi wao kutokana na changamoto za kifedha. Kwa kulipia ada hizo, Airtel Divas wamewawezesha wagonjwa hao kuendelea na kliniki.
Akizungumza wakati wa kupokea msaada huo, Merikiori Niniko, Meneja wa Huduma za Ustawi wa Jamii wa ORCI, alisema kuwa taasisi hiyo inakabiliwa na mahitaji makubwa kutokana na matibabu ya saratani kuwa mrefu na changamoto zinazohitaji msaada wa kila siku.
“Taasisi yetu inaendelea kukabili mahitaji makubwa kwa sababu matibabu ya saratani yanahitaji ukaguzi wa muda mrefu. Wagonjwa wengi hukosa au kuchelewesha ukaguzi wao kwa sababu hawawezi kulipa ada za kliniki. Tunashukuru sana Airtel Divas kwa kulipia gharama za zaidi ya wagonjwa 40, ili waweze kuendelea na ukaguzi wao muhimu wa afya,” amesema Niniko.

Kwa upande wake, Jemima Masimba, Mwenyekiti wa Airtel Divas, amesema kuwa airtel Diva’s waliguswa na changamoto zinazokabiliwa na wanawake waliomaliza matibabu ya saratani lakini wanashindwa kuendelea na ukaguzi wao wa kawaida.
“Tumeguswa sana na hadithi za wagonjwa ambao hawawezi kuhudhuria ukaguzi wao wa kliniki kutokana na changamoto za kifedha. Ukaguzi huu ni muhimu sana kwa afya yao na katika safari yao ya kupona. Kama Airtel Divas, tuliona ni wajibu wetu kulipia ada zao ili kila mwanamke aweze kuendelea na huduma muhimu za afya,” amesema Masimba.
Juhudi hii ni sehemu ya mpango mpana wa Airtel Tanzania wa kusaidia jamii, kukuza afya ya wanawake, na kuhakikisha makundi yenye uhitaji wanapata huduma muhimu. Kupitia Airtel Divas, wafanyakazi wanawake wa kampuni hiyo wanaendelea kuongoza miradi yenye athari chanya kwa jamii na kutoa msaada kwa walio hatarini.

More Stories
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako
TTCL yaadhimisha siku ya Wanawake kwa kutoa msaada JKCI
Wananchi Dodoma washauri TBA kujenga nyumba za kupangisha watu binafsi