October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Matukio zaidi ya 8,700 yameripotiwa jana, idadi inayoelemea uwezo wa utolewaji huduma za afya kwa umma nchini Afrika Kusini. (BBC)

Afrika Kusini waandaa makaburi milioni 1.5 ya corona

Gauteng, Afrika Kusini

MAOFISA wa afya katika Jimbo la Gauteng nchini Afrika Kusini ambako ndiko kunaongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona, wamesema kuwa mamlaka za nchi hiyo zinaandaa maeneo yenye makaburi 1,500,000 wakati visa vya janga hilo ambavyo vimedhibitishwa vinaendelea kuongezeka.

Bandile Masuku, daktari mwandamizi ambaye ni mjumbe wa baraza la utendaji jimboni humo, amekaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ilikuwa ni jukumu la umma kuhakikisha kutokuwepo kwa  makaburi hayo.

 “Ni majadiliano ambayo wanajamii wanajisikia vibaya,” alinukuliwa akisema.

Jimbo la Gauteng linajumuisha majiji ya Johannesburg na Mji Mkuu wa nchi hiyo, Pretoria. Idadi ya matukio yanayohusu virusi vya Corona jijini humo sasa inazidi 71,000, ama asilimia 33 ya visa vyote Afrika Kusini.

Nchi hiyo ina zaidi ya visa 215,000 vilivyothibitishwa, na inatuma baadhi ya taarifa zenye idadi kubwa zaidi duniani za visa vipya vilivyoripotiwa. 

Wakati huo huo, ulegezaji hatua za kudhibiti covid-19 maarufu ‘lockdowns’ nchini humo unaendelea.