Na Mutta Robert,TimesMajira Online,Geita
SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limeanza kusambaza umeme unaotoka kwenye kituo kipya cha kupooza na kusambaza umeme cha Mpomvu Mjini Geita baada ya kuwashwa rasmi jana na Mkuu wa Mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel.

Kituo hicho kinapokea umeme wa msongo wa Kilovoti 220 kutoka Bulyanhulu na kuupoza hadi Kilovoti 33 kwa ajili ya kuusambaza kwa watumiaji mbalimbali.
Kituo hicho kimejengwa kwa gharama ya Bilioni 50 ambacho umeme utakaotoka kwenye kituo hicho utakuwa na uhakika na kumaliza tatizo la umeme katika Mkoa wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel akiwasha kituo hicho, amesema tatizo la umeme katika Mkoa huo limepataiwa ufumbuzi.
Amesema kuwa malalamiko ya wateja wa umeme hasa wawekezaji kwenye sekta ya madini ,viwanda na watumiaji wa kawaida yamepata suluhisho.

More Stories
Programu ya Mama Samia yarasimisha ujuzi
TCDC kuzindua kampeni kuimarisha Ushirika
TPHPA kung’arisha Mei Mosi Njombe