Na Mwandishi Wetu,Timesmajira
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (INEC) imekanusha madai yanayosambaa mitandaoni kwamba mfumo wake wa uchaguzi umeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na chama cha siasa.
Taarifa liyotolewa leo,Agosti 23,2025 INEC imesema madai hayo ni ya uongo na upotoshaji, ikisisitiza kuwa mfumo wa uchaguzi nchini unatumia njia za kawaida (manual) na hauna uhusiano wowote wa kielektroniki na taasisi za serikali au binafsi.
“Daftari la kudumu la wapiga kura halijaunganishwa na mfumo wowote. Utaratibu wa kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo unafanywa kwa njia ya kawaida,”Ilisema taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhani Kailima.
Tume ilibainisha kuwa wapiga kura hutumia kadi ya kupigia kura pekee, siyo Kitambulisho cha Taifa, na majina yao husomwa hadharani kituoni kabla ya kuruhusiwa kupiga kura. Vyama vya siasa na mawakala wao pia walikabidhiwa daftari la wapiga kura baada ya uboreshaji.
INEC imewataka wananchi kupuuza taarifa hizo na kufuatilia chanzo rasmi cha tume, ikiwemo tovuti yake na kurasa za mitandao ya kijamii, kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.



More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako