Na Zena Mohamed,Timesmajiraonline,Dodoma
MWAJUMA Mirambo anakuwa mgombea wa nane kuchukua fomu Tume Hurubya Taifa ya Uchaguzi(INEC) za kuomba kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti cha Rais akiwa na mgombea mwenza Mashavu Alawi Haji kutoka Chama cha Union for Multiparty Democracy(UMD).
Mirambo amekabidhiwa mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi,Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele jijini hapa leo,Agosti 11,2025.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu hizo Mirambo amesema kuwa tukishinda watahakikisha wanasimamia vizuri Uchumi wa nchi ikiwemo kukusanya kodi vizuri.
“Tunajua serikali kazi yake kubwa ni kukusanya mapato ya kodi,tutahakikisha tunakusanya kodi vizuri ili tuweze kutimiza majukumu ambayo tumejiwekea watanzania waweze kuona raha kuishi kwenye nchi yao,”amesema.
Amesema kuwa UMD wapo tayari kuanza harakati za uchaguzi na wao wanasera ambazo ni wezeshi kwa watanzania ambazo ni rafiki na ambazo zitamgusa kila mtanzania katika kuhakikisha wanainua Uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini uchumi wa Taifa kwa ujumla.
“Sisi kama UMD tunaomba watanzania watuunge mkono katika kutupigia kura itakapofika wakati wa kupiga kura kwasababu vipaumbele vyetu ni rafiki kwa kila Mtanzania,Mwanamama,Kijana,Makundi maalum,wafugaji na wakulima.
“Sera za UMD tunaamini katika sera za majimbo katika kuwa na sera za majimbo tunaamini kila Mtanzania pale alipo ataweza kufurahia uchumi uliopo kwenye eneo lake na kwenye Taifa
Hatutajutia watanzania kuzaliwa Tanzania,”amesema.
Aidha amesema kuwa wanajua changamoto za watanzania kuwa ni zile zile ambazo amezitaja,Afya,Elimu,Maji na Miundombinu hivyo wao wakishinda watahakikisha wanzishughulikia ili hata mtoto anayezaliwa Tanzania aone amezaliwa sehemu sahihi.






More Stories
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako
TTCL yaadhimisha siku ya Wanawake kwa kutoa msaada JKCI
Wananchi Dodoma washauri TBA kujenga nyumba za kupangisha watu binafsi