March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

NIT wanadi kozi ya urubanimaonesho ya Sabasaba

Na Mwandishi wetu,TimesmajiraOnline,

CHUO cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimewakaribisha vijana kufikia katika Banda lao lililopo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Sabasaba(DIFT) ili wapate elimu ya kina kuhusu kozi ya Urubani.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho hayo  Mkufunzi wa Urubani kutoka Chuo hicho, Ashrafa Ramadhan amesema chuo hicho tayari kimeishaanza  rasmi kutoa mafunzo ya urubani kwa vitendo kwa vijana wa kitanzania.

“Mafunzo Urubani tayari  yameanza kutolewa  na wanafunzi wa kwanza 10 wamejiunga, wakiwemo wanawake wanne na wanaume sita tunavyo vifaa vya kisasa na wataalamu waliobobea katika nyanja hiyo”amesema

Ramadhan amesema NIT imejipanga vizuri kuanzia hatua za awali za kumfundisha Mwanafunzi kuanzia ardhini hadi mafunzo ya angani.

Akitaja sifa za kujiunga na mafunzo hayo amesema  ni kuanzia elimu ya kidato cha nne, na umri wa kuanzia miaka 17 na kuendelea.

Aidha amesema  kuwa NIT imewekeza katika miundombinu na teknolojia ya kisasa ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mafunzo bora ya kitaalamu na ya kimataifa.