March 8, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mwakyembe arejesha fomu ya kuomba ubunge Jimbo la Temeke

Na Bakari Lulela ,Timesmajira

DIWANI mstaafu wa kata ya mtoni na kada wa chama cha Mapindizi (CCM) mh Bernard Mwakyembe  Leo ni siku muhimu kwake akirejesha fomu ya kugombea kiti cha ubunge katika Jimbo la Temeke jijini Dar es salaam.

Akizungumza jijini na waandishi wa habari wakati akirejesha fomu mgombea huyo amesema kuwa wengi watastaajabu kwanini amegombea kiti hicho cha ubunge ilihali mwaka 2020 aliwahi kuwa kampeni meneja wa mbunge wa Temeke.

“Kimsingi uchaguzi huchukua muda wa miaka mitano hivyo Dada Rose amefanya yaliyo ya kwake na amemaliza na sasa naingia Mimi nifanye yanayostahiki kuyafanya naomba mungu anijaalie,” amesema  Mwakyembe 

Aidha mgombea huyo ametaja vipaumbele vyake endapo akipata ridhaa ya kuchaguliwa ikiwa ni pamoja na kujenga miundombinu ya Barabara, masoko na kuhakikisha vijana wanapata fursa za ajira zilizo rasmi.