Fresha Kinasa TimesMajira Online Mara.
MBUNGE anayemaliza muda wake wa Jimbo la Bunda Boniphace Mwita amerejesha rasmi fomu aliyochukua ya kuwania kutetea kiti chake kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Mwita, amerejesha fomu hiyo Julai Mosi 2025 kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda Evodia Edward, Ambapo aliichukua Juni 28, 2025.
Aidha, Mwita ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Hassan kwa fedha nyingi za maendeleo alizotoa ambazo zimeleta maendeleo katika sekta mbalimbali.
Huku pia akisema, shauku yake ni kuendelea kuwatumikia Wananchi waJimbo hilo iwapo atapata ridhaa ya kuteuliwa kugombea na kushinda nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo.

More Stories
Senyamule:Serikali inapaswa kuzitambua Kampuni zinazofanya biashara ya ardhi
Serikali kuendelea kupanua fursa elimu Singida
Kumekucha CDF Cup 2026, NMB yaweka Sh milioni 150