March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Boniphace Mwita arejesha fomu kutetea kiti chake jimbo la Bunda

Fresha Kinasa TimesMajira Online Mara. 

MBUNGE anayemaliza muda wake wa Jimbo la Bunda  Boniphace Mwita  amerejesha  rasmi fomu aliyochukua ya kuwania  kutetea kiti chake kupitia Chama Cha Mapinduzi.

Mwita, amerejesha fomu hiyo Julai Mosi 2025 kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda Evodia Edward,  Ambapo aliichukua Juni 28, 2025.

Aidha, Mwita ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Hassan kwa fedha nyingi za maendeleo alizotoa ambazo zimeleta maendeleo katika sekta mbalimbali.

Huku pia  akisema,  shauku yake ni kuendelea kuwatumikia Wananchi waJimbo hilo iwapo atapata ridhaa ya kuteuliwa kugombea na kushinda nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo.