March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Waislamu watakiwa kutumia mwaka mpya wa kiislamu kutafari maisha ya Mtume 

*Kwa ajili ya kuleta haki, amani na mshikamo kwa jamii.

*CCM yawatakia watanzania wote heri ya kuukaribisha mwaka mpya wa kiislamu leo

Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online

CHAMA Cha Mapinduzi ( CCM) kinatoa salamu za heri na baraka kwa waislamu wote nchini na duniani kote katika kuukaribisha mwaka mpya wa kiislamu 1447 muharram.

Akitoa salamu kwa niaba ya chama hicho, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema mwaka huu mpya wa kiislamu ni fursa  kwa wauminu wa duni hiyo   kutafakari maisha ya Mtume Muhammad ( S. A. W), hususani ujasiri wake, uvumilivu na moyo wa kujitolea kwa ajili ya kuleta haki, amani na mshikamo kwa jamii.

” Kwa niaba ya CCM na kwangu binafsi nawatakia waislamu wote mwaka mpya uliojaa mafanikio, afya nje, amani na mshikamano.Tunathamini mchango wa jamii ya kiislamu katika kujenga taifa letu, kukuza maadili, kuimarisha uzalendo na kudumisha utaifa”, amesema Balozi Nchimbi. 

Aidha ametoa wito kwa watanzania wote, bila kujali tofauti za kidini, kuuenzi mwaka huu kwa kudumisha misingi ya mshikamano wa kitaifa, kuvumiliana na kushirikiana katika kujenga taifa katika misingi ya haki na maendeleo endelevu.

Hata hivyo amesisitiza kuwa chama hicho  dhamira yake ni kuendelea kushirikiana na wananchi katika kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa nchi ya amani, umoja na maendeleo kwa wote.