Na Heri Shaaban, Timesmajira Online,Ilala
MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Karume wilayani Ilala jijini Dar,Hajji Bechina,ametoa chakula kwa ajili ya sikukuu ya Eid kwa wananchi 560 vyenye thamani ya milioni 10.
Akizungumza katika tukio hilo Bechina,amesema ametoa sadaka hiyo kwa wananchi na makundi maalum.Ambapo kila mwaka amekuwa alifanya hivyo
Sanjari na hayo alikabidhi runinga ya inchi 46 kwa vijiwe viwili vya Young Star na Wachonga vinyango vyote vya Ilala,huku akiwahimiza wananchi kuchagua wagombea wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi(CCM), katika uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika mwaka huu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ilala, Said Sidde,amewahimiza Wenyeviti na viongozi wengine kuiga mfano wa Mwenyekiti huyo wa kuwajali wananchi wake.
More Stories
Wataalamu wabobezi katika sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi wakutana nchini
Wizara ya afya yachukua hatua sakata la Mzazi anayedai kubadilishiwa Mtoto Arusha
EWURA yatangaza bei za Mafuta kwa mwezi Aprili 2025