Na Hadija Bagasha, Timesmajira Online, Tanga
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt.Batilda Burian,amesema wameanza mazungumzo na Hazina kuangalia uwezekano kwa waliopewa viwanda na kuvitelekeza kuwanyang’anya ili wapewe watu wenye uwezo wa kuviendeleza na sio kuacha magofu.
Balozi Batilda ameyasema hayo Februari 12,2025, wakati akizungumza na Viongozi wa dini na vyama vya siasa mkoani Tanga, ambapo amesema Mkoa huo umeanza mchakato wa kuvifufua viwanda vilivyokufa na hawataki kuona magofu.
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2025/02/IMG-20250213-WA0019.jpg)
Amesema,Tanga kulikuwa na viwanda vingi ambavyo vinafanya kazi ikiwemo kiwanda cha nondo,misumari,mbao na foma ambavyo watu walivichukua na kivitelekeza.
“Kwa Sasa tupo kwenye mazungumzo na hazina kuangalia uwezekano waliopewa hivyo viwanda wanyang’anywe na wapewe watu wengine,benki zipo, vijana wapo, BBT ya mama Samia jenga kesho iliobora ipo ambayo inawawezesha vijana waingie kwenye uwekezaji, mifugo,uvuvi, kilimo hata viwanda,”amesema Balozi Batilda.
Pia amewaomba viongozi wa dini kuhamasisha waumini kijitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ikiwemo kuboresha taarifa zao,ambapo zoezi hilo linaanza Februari 13 hadi 19,2025.
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2025/02/IMG-20250213-WA0012-1024x576.jpg)
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2025/02/IMG-20250213-WA0013-1024x576.jpg)
More Stories
Shaka:Uimara wa Rais Samia ni matokeo chanya unaojali kesho ya nchi
Ajira mpya Muhimbili wahimizwa kutoa huduma bora kwa wananchi
TMA:Kuna ongezeko la joto kwa baadhi ya maeneo nchini