Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Januari 06, 2025 amekabidhiwa Jezi ya Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Zanzibar (Zanzibar Heroes).


Mheshimiwa Othman ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa ACT- Wazalendo amekabidhiwa Jezi hiyo, kutoka kwa Naibu Waziri Kivuli wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, wa Chama hicho, Ndugu Humoud Ahmed Said, hapo Ofisini kwa Makamu wa Kwanza wa Rais, Migombani Mkoa wa Mjini-Magharibi, Unguja.

More Stories
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka
BAKWATA yawazawadia washindi wakuhifadhi Qur’an