Na Mwandishi wetu, timesmajira
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kinondoni SACP Mtatiro Kitinkwi akiambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule wameongoza hafla fupi ya kupokea pikipiki tatu aina ya HERO kutoka kampuni iitwayo DOUGH WORKS ambao ni wamiliki wa migahawa ya KFC nchini.

Akizungumza baada ya kupokea Pikipiki hizo Mkuu wa Wilaya,SACP Kitinkwi aliushukuru uongozi wa Kampuni hiyo kwa msaada huo kisha kuzikabidhi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni na kupokelewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Akipokea msaada huo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni amemshukuru ,Mkuu wa wilaya na Mmiliki wa Kampuni hiyo kwa kutambua na kuthamini jitihada katika kupambana na kuzuia uhalifu na kwamba pikipiki hizo zitaenda kusaidia kuimarisha doria kwenye maeneo yenye uhitaji wa pikipiki.
More Stories
Papa Francis afariki Jumatatu ya Pasaka akiwa na miaka 88
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni