Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewasili mkoani Shinyanga akitokea jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi Desemba 29, 2023.

Alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kahama, Dkt. Biteko alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM)mkoani Shinyanga akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi, Mbunge wa Ushetu, Emanuel Cherehani na Mbunge wa Kahama Mjini, Jumanne Kishimba.


More Stories
Ussi awataka wananchi Handeni kulinda miundombinu ya maji
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025