Na Heri Shaaban , TimesMajira Online
Mjumbe wa Baraza la Wazazi CCM Taifa SAADY KHIMJI anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Jakaya kikwete kata ya Segerea Mkutano huo utafanyika September 30 mwaka huu .
Akizungumza na waandishi wa habari Katibu wa Wazazi Jakaya kikwete Heri Shaaban alisema mkutano huo unatarajia kuanza saa tatu asubuhi katika viwanja vya Janguo ambapo wanachama wa chama cha MAPINDUZI CCM na Jumuiya ya Wazazi wote wanakaribishwa siku hiyo kwani kutakuwa na matukio mbali mbali

Aidha pia katika mkutano mkuu huo mgeni Maalum anatarajia kuwa Mjumbe wa Baraza la Jumuiya ya Wazazi mkoa Dar es Salaam Abdulkarim Masamaki na viongozi mbali mbali wa wilaya kutoka Jumuiya ya Wazazi.
More Stories
Dkt.Samia; Meatu mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo nishati
REA yaendelea kusambaza Nishati Bora kwa wananchi,yamshukuru Rais Dkt.Samia
Vivo Energy Tanzania, yazindua Kampeni ya “Uliza Oili ya Shell”