Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Balozi Ali Idi Siwa, amefungua Mkutano wa 50 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NSSF.
Katika Mkutano huo, Balozi Siwa alisisitiza uboreshaji wa huduma bora kwa wanachama, kuendelea kuwajengea uwezo wafanyakazi, kuongeza kasi ya ukuaji wa Mfuko kwa kuifikia sekta binafsi na sekta isiyo rasmi na kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utendaji kazi.
Lengo la mkutano huo ni kupitia Mpango wa mwaka ujao wa fedha na bajeti kwa mwaka 2023/2024, ikiwa ni ushirikishwaji wa wafanyakazi katika maamuzi ya kiutendaji. Ufunguzi wa mkutano huo umefanyika tarehe 18 Aprili 2023 katika ukumbi wa AICC jijini Arusha.
More Stories
Benki ya NMB yapiga jeki Zahanati ya Kijiji cha Ivilikinge Wilyani Makete
Wanawake, vijana watakiwa kuchangamkia fursa za zabuni
CCM Zanzibar yapongeza hotuba ya Dkt. Rais Samia