Na Joyce Kasiki, TimesMajira,Online, Dodoma
RAIS John Magufuli anatarajiwa kulihutubia Bunge Ijumaa, hotuba ambayo inatarajia kuonesha dira ya Serikali yake katika kipindi uongozi wake wa pili cha miaka mitano katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Kupitia hotiba hiyo Rais Magufuli anatarajia kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ratiba ya Rais Magufuli kuhutubia Bunge imetolewa leo na Spika wa Bunge, Job Ndugai wakati akizungumza bungeni kuhusu utaratibu utakavyokuwa kesho kutwa.
“Hotuba hii ni muhimu, lakini kupitia sisi wabunge anakuwa analihutubia Taifa, kwa hiyo naomba niwataarifuni kuwa kesho kutwa saa tatu kamili asubuhi tutawaomba waheshimiwa wote tuwe ndani ya ukumbi huu,” amesema Spika Ndugai.

More Stories
Ujuzi wa Wezesha Binti wawasaidia vijana kujiajiri na kupata ajira
Nombo: Tanzania yaandaa vijana kushindana kimataifa
TVET yatajwa nguzo ya Uchumi kuelekea Dira 2050