September 29, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mwamko wanawake wadhihirisha wakipewa nafasi wataweza

Na Bakari Lulela,TimesMajira Online

KUTOKANA na mwamko wa wanawake kujitokeza kushiriki masuala ya kugombea uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, imedhihirika wakipewa nafasi, wataweza kuonesha vipawa vya hali ya juu vitakavyoleta mabadiliko chanya kwenye ukombozi wa taifa.

Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA), Tike Mwambipile kwenye semina maalumu iliyokuwa ikiwajengea uwezo wanahabari namna ya kuandika ama kuripoti, taarifa zinazowahusu wanawake katika kufikia malengo yao hususan ya uongozi.

“Wanawake wana uwezo mkubwa katika kukabiliana na masuala mbalimbali ya uongozi ndani ya taifa, ambapo wakipatiwa nafasi wataweza kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii zetu,” amesema Mwambipile.