Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online-Ilala
MKUU wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, amewataka Madiwani wa Halmashauri ya jiji la Dar-es-Salaam, kufanya kazi kwa kushirikiana na Watendaji na Wenyeviti wa Serikali za mitaa katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi
Mpogolo, amrsema hayo wilayani Ilala ,wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar-es-Salaam.

“Nawaomba Madiwani wangu wa Halmashauri ya Jiji mkawe kiunganishi baina yenu na Watendaji pamoja na Wenyeviti wa Serikali za mitaa,katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ili tumsaidie Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan,”amesema Mpogolo.
Pia amewataka Madiwani kushuka chini ngazi ya mtaa kwa kushirikiana na watendaji na Wenyeviti ndio kwenye kero kubwa kwa kuweka vikao vya utatuzi wa kero na mikutano ya wananchi.
Sanjari na hayo amewataka kutumia mafunzo kwa tija kwa ajili ya kuwatumikia wananchi katika maeneo yao kwani wakifahamu shida za wananchi hawawezi kuona mzigo kuwahudumia.
Aidha amewataka Madiwani hao kusimamia ukusanyaji mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar-es-Salaam ili Serikali iweze kufikia malengo pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kuu



More Stories
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako
TTCL yaadhimisha siku ya Wanawake kwa kutoa msaada JKCI
Wananchi Dodoma washauri TBA kujenga nyumba za kupangisha watu binafsi