Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Eng. Anthony Sanga amewasili katika Kijiji cha Gendabi Wilaya ya Hanang pamoja na wataalamu ya Wizara kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya maafa yaliyoasababishwa na mvua kubwa inayoendelea kunyesha Nchini kote.
Aidha Eng. Sanga ameunda timu ya Wataalamu mbalimbali itakayofanya kazi ya tathmini ya maafa hayo kufuatia maporomoko ya magogo,mawe na matope yaliyosababishwa na mvua, zinazoendelea kunyesha hapa nchini.
Pamoja na mambo mengine timu hiyo ya wataalamu itafanya tathimini ya kiwango cha uharibifu wa mali,makazi na Shughuli za wananchi.
Hatua hii ya Katibu Mkuu Sanga kutekeleza maagizo ya haya Waziri Mkuu ya kuitaka serikali kufanya tathmini ya hali maafa ili wananchi waliokumbwa na maafa waweze kutokana na madhara yaliyosababishwa mafuriko hayo.

More Stories
Ussi awataka wananchi Handeni kulinda miundombinu ya maji
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025