Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Benki ya NMB imepata nafasi ya kutembelewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na wenye Mahitaji Maalum – Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima katika ofisi zao za Makao Makuu jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB – Ruth Zaipuna aliembatana na Afisa Mkuu wa Fedha NMB – Juma Kimori, amempokea Mhe. Gwajima na kumuelezea kuhusu masuluhisho yanayogusa moja kwa moja makundi mbalimbali katika jamii.

Lakini pia, aliahidi kushirikiana na serikali kuhakikisha masuluhisho yao yanakuwa chachu ya maendeleo kwa makundi yote katika jamii kwa kuendelea kuwekeza kwenye teknolojia na ubunifu.

Katika salamu zake, Mhe. Gwajima alimpongeza Afisa Mtendaji Mkuu wetu pamoja na uongozi mzima wa Benki wa NMB kwa mafanikio waliyoyapata, na kuahidi kuna balozi mzuri kufikisha fursa zinazotolewa na benki hiyo kwa wananchi ili waweze kujijenga kiuchumi.
More Stories
Wanaodaiwa kufukua kaburi na kuondoka na mwili wa marehemu watafutwa
Kituo cha afya Kisiwa cha Rukuba chafungiwa umeme jua kurahisisha huduma
Kapinga:Wakandarasi wasimamiwe kutekeleza miradi ya nishati kwa wakati