Na Mwandishi Wetu,Timesmajira
WASHTAKIWA waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka ya kumbaka na kumuingilia kinyume na maumbile binti wa Yombo Dovya, jijini Dar es Salaam wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Hukumu hiyo imetolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma leo baada ya kuwatia hatiani kwenye mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili.
Washtakiwa ambao kwenye video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii wakati wakifanya unyama huo wakidai wametumwa na afande walikuwa wanakabiliwa na kesi ya jinai namba 23476 ya mwaka 2024.
Waliohukumiwa adhabu hiyo ni MT 140105 Clinton Damas, maarufu Nyundo ambaye ni askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), askari Magereza C.1693 Praygod Mushi, Nickson Jackson ‘Machuche’ na Amin Lema anayejulikana pia kwa jina la Kindamba.
Pamoja na hukumu Mahakama hiyo imewataka kila mmoja kumlipa binti huyo fidia ya sh. milioni moja

More Stories
DC Mbozi afuturisha wananchi, asisitiza mshikamano na Umoja.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Nina imani mubna utendaji kazi wa ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria
Tanzania yaelekezwa kuongeza ushiriki katika biashara ya kaboni kimataifa.