Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake kwa wadogo anaipeleka kwa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa yeye ana utashi wa kisiasa ya kutaka kuona sekta ya uzalishaji inasonga mbele.
Ulega amesema hayo kwenye Mkutano wa Wavuvi Wadogo Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 5-7,2024.

Mapema leo katika mkutano huo, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Afrika linaloshughulikia Tafiti, Haki za Wanyama na sekta ya Uvuvi (AU-IBAR), Bi. Hellen Guebama alimkabidhi tuzo Waziri Ulega ikiwa ni ishara ya kumpa heshima na kutambua mchango wake kwenye shughuli za uvuvi mdogo nchini.
More Stories
Yas yaja na ‘Anzia Ulipo’ kuhamasisha watanzania kusimamia ndoto zao
Coca-Cola Kwanza kuwanufaisha mama lishe Stendi ya Msamvu Marogoro
Sheikh Ponda akabidhiwa kadi ya heshima ya Maalim Seif