Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema wameazimia kuweka mazingira yatakayofanya biashara kati ya Tanzania na Zambia zisiwe na vikwazo.
Wakizungumza katika Kongamano la Wafanyabiashara wa Tanzania na Zambia lililofanyika jana jioni marais hao walisema eneo moja la muhimu ni kuhakikisha magari hayakai kwenye mipaka kwa muda mrefu pasi na sababu.
Marais hao wanakutana kwenye mkutano wa ana kwa ana leo asubuhi na waliwaambia Wafanyabiashara hao kwamba mazungumzo yao yatajikita kwenye kuweka taratibu za kuondoa changamoto hizo.





More Stories
TMDA yajivunia kuanzisha mfumo thabiti wa udhibiti wa vifaa tiba na vitendanishi
Kikwete kuungana na marais watatu kushiriki Kongamano la nane la viongozi Afrika
Katavi yazindua kampeni kukabiliana na udumavu